SHTUKA MREMBO: MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA KUTENDWA NA UMPENDAE...!

WEKA TANGAZO

KATIKA MAISHA YA KIMAPENZI HAKUNA KITU KINACHOUMA KAMA KUSALITIWA, TENA KUSALITIWA KUNAKOUMA ZAIDI NI PALE UNAPOBAINI MPENZI WAKO KAMPA PENZI MTU UNAYEMJUA HALAFU UKIJILINGANISHA WEWE NA HUYO ALIYEPEWA UNASHINDWA KUELEWA KILICHOMSHAWISHI MPENZI WAKO KUMPA PENZI HUYO MTU...

Niseme tu kwamba wapo wachache waliotulia ila asilimia kubwa ya walio kwenye uhusiano ni wasaliti hata tafiti zimethibitisha hilo. Kama hali yenyewe iko hivyo, cha kujiuliza ni kwamba unapobaini mpenzi wako kakusaliti ni kipi unachotakiwa kufanya? Je, ni kuamua kunywa sumu kama ambavyo wamekuwa wakifanya wengine? Sidhani kama huo ni uamuzi sahihi. 

Yafuatayo baadhi ya mambo ambayo unapaswa kuyafanya baada ya kubaini kuwa mpenzi wako amekusaliti. 

Kubaliana na kilichotokea 

Kama keshakusaliti ni tukio ambao limeshatokea na haliwezi kufutika. Kubali kuwa umetendwa, huzunika lakini mwisho liache lipite ili uweze kujipanga upya. 
Usijilaumu 
Wapo ambao wakishasalitiwa hujuta kukubali kuingia kwenye uhusiano na watu waliowatenda. Utamsikia mtu akisema “najuta kumkubalia awe mpenzi wangu”. Kujilaumu kwa namna hiyo hukutakiwi kwani kutakufanya uzidi kunyong’onyea. 
Jitoe 
Jifanye kama vile aliyesalitiwa siyo wewe bali ni rafiki yako kisha jiulize ungemshaurije? Ushauri ambao ungempa basi uchukue kisha uufanyie kazi.  
Pima ulivyoathirika 

Je, kitendo cha mpenzi wako kukusaliti kimekukosesha imani juu yake? Kama ni hivyo, unadhani una sababu ya kuendelea kuwa naye au unahisi madhara aliyokupatia huwezi kumvumilia? 



Mweleze ukweli 

Kwa vyovyote utakavyoamua ni lazima umweleze ukweli juu namna alivyokuumiza kwa usaliti wake. Hata kama utampa nafasi nyingine lazima ajue jinsi alivyokuumiza ili iwe changamoto kwake. 
Chunguza kwa nini kakusaliti 
Usiliache likapita hivi hivi, unatakiwa kujua sababu ya yeye kukusaliti. Je, kuna ambacho anakikosa kwako au ni tamaa zake tu? Jibu utakalolipata litakusaidia katika maisha yako ya kimapenzi. 
Usikubali akulainishe 
Huenda huyo mpenzi wako ni msanii na anaweza kukulainisha kwa maneno ambayo yanaweza kukufanya ukalichukulia tukio hilo kiurahisi. Kuwa na msimamo na eleza hisia zako kwa uwazi. 
Amua kusuka au kunyoa 
Likishatokea hilo jaribu kuzungumza na moyo wako. Uamuzi wa kuendelea kuwa naye au kumuacha uuchukue bila shinikizo. Hata kama kakuumiza, kama unadhani unaweza kumpa nafasi nyingine mpe ili usije ukajuta baadaye kwa kumkosa lakini kama unaona moyo wako unamkataa, muache.
WEKA TANGAZO

0 maoni: