Mume wangu anawashwa sehemu zake za siri

WEKA TANGAZO

Mimi ni dada niliyeolewa na nimebahatika kupata mtoto mmoja katika ndoa yangu na ana miaka 3, ila toka nimjue mume wangu, uwa anawashwa sehemu zake za siri, na tukiwa tumelala usiku utamsikia anajikuna tena kwa nguvu, ni kijaribu kuongea nae twende kwa dokta wa ngozi hataki, anasema nikawaida tu, ila mi ananiboa kitu kimoja anatoka kujikuna harafu anamshika mtoto bila kunawa.

Naombeni ushauri, au kama kuna dawa ya kupaka naweza nikanunua nikajaribu kumpaka, nampenda mume wangu ndo maana najaribu kutafuta njia mbadala
WEKA TANGAZO

0 maoni: