STORY:THE WORLD IZ NOT FAIR MTUNZI: CHICOLOVE NAMBA: 0658,0765,270133 SEHEMU: 4

WEKA TANGAZO
Eeh mzee uyu si kama tu mtoto wako inakuaje unamwita mpenzi?
"Kila mtu akabaki akinishangaa! Hata yule binti nae akaona aibu akawa anatazama chini tu uku akiwa anabinyabinya simu yake!!
"Mustapha akawa analakufanya zaidi tu ya kuniangalia kwa hasira na kuamuru fundi afunge kazi uku akapanda kwenye gari na yule binti akaondoka!!

"Acha mafundi waanze kuniletea shida ooh wewe umemkasirisha bosi sasa utatulipa pesa zetu leo!
"Wengine wakawa wananitukana nakutoa maneno makali dhidi yangu nakunifanya niingie hofu zaidi itakuaje hapa nishalikoroga napaswa nilinywe!
"Oyaa ninyi acheni kumsumbua dogo kama angekua ni mtu wa kutoa hela angetoa ndio aondoke sio mnashushia lawama tu"

Mara gafla Mustapha akarudi uku akiwa na jazba akanisogelea na kuninasa bonge la kofi adi nikaanguka!
"Pumbavu kabisa wewe mtoto ujui yule ni nani unaropoka ropoka tu namjali sana yule binti kuliko mke wangu!
"Nikainuka pale chini uku machozi yakinitirika nikajikuta nasema Samahani mzee!
"Akabaki tu ananiangalia kama chui uku macho yakiwa makali kama kaa la moto!
"Akampa fundi maagizo kisha akaondoka zake nikachukua rambo langu la nguo nakuanza safari yakurudi nyumbani uku nikiwa na mawazo sana nitakula nini!

Nikiwa njiani na mawazo yangu nitakula nini mara gafla nakoswa na gari nakufungia break miguuni mwangu!
"Akashuka kijana mmoja sharobaro uku akiwa anafoka na kunitukana kwa kingereza akanikwida!
"Na kuniambia you bitch are you want to die?
"Nikabaki tu naangaza macho sikujua hata nimjibu nini?
"Fuck you son of bitch akapanda gari nakuwasha akanisukuma na side mirror nikaangukia uko kwenye mtaro!
"Niliumia sehemu za magoti sana uku kila mahali nikihisi maumivu nikiwa najitaidi kujikongoja nitoke mule kwenye daraja!
Gafla lile gari likarudi tena kwa kasi nakupaki pembeni akashuka binti mmoja na yule kijana wakiwa wanazozana sana kama vile wamegombana!
"Yule binti akanisogelea na kunisalimia kaka habari yako?
"Salama dada! Umeumia sana?
"Sio sana ila nasikia maumivu kila mahali kwani wewe ni nani?
"Haya umeshamuumiza kijana wa watu mchukue mpeleke hospitali lasivyo hatuelewani hapa!
"Yule dada pamoja na urembo na uzuri wake akashuka kule kwenye mtaro wa maji machafu na kunishika mköno kunisaidia kutoka kule!
"Nikajikuta mawazo yangu yanaenda mbali sana nikawa namshangaa tu usoni uku yeye akiwa anajitaidi kunibeba uku uso wake ukionesha kuwa na wasiwasi dhidi yangu!
"Nikiwa nimeendelea tu kuduwaa uku nimemtazama machoni mwake!

"Yule sharobaro akashtuka na kusema hakika ninyi watu mtakuwa...............ITAENDELEAAA!
WEKA TANGAZO

0 maoni: