STORY: THE WORLD IZ NOT FAIR MTUNZI: CHICOLOVE JR NAMBA: 0658,0765,270133 SEHEMU: 15

WEKA TANGAZO
Mama basi tule nina njaa! nikajitaidi kupotezea maana mama kama tayari alisha hisi jambo fulani kati yangu na Aurelia"
Moses alikua anacheka tu uku Aurelia akiwa anaona aibu aibu ivi"
"Mama akiwa anatutazama uku akiwa anatabasamu nakunifanya nicheke"
"Nini mama mbona unatutazama unacheka kuna tatizo mama yangu nakupenda"
Hata nami nakupenda mwanangu ila kumbuka nimeanza kuona jua kabla yako!
"Eeeh unamaana gani kusema ivyo mama mbona sikuelewi alafu mama leo nataka nikalale kwa akina Moses!
"Ebu niache kwanza nipakue chakula maneno mengi tu"
* * * Nisikilize mpenzi wewe unawanawake wengi uyo aliyekupigia simu ni nani?
"Cwty dada yangu wa uko kijijini ndio amepiga alikua ananipa habari za nyumbani"
"Siunajua tena wazazi nao wakipata vocha basi wanasumbua sumbua mpenzi"
"Hata sitaki kukusikiliza unaongea uongo ambao unajidhirisha kweli utaonaje aibu kuongea na dada yako mbele yangu kama sio wanawake zako unafikiri mimi mpumbavu juzi umekuja na lipshine mdomoni nikanyamaza tu"
"Ulijipaka wapi kama ukua na mwananke mwingine?
"Sikiliza Mustapha wewe unaona pesa zako ndio kigezo cha kufanya upumbavu wako sasa wengi sisi atuhitaji pesa tunahitaji mapenzi ya kweli"
"Mustapha akiwa amewekwa kitimoto na mmoja wa wanawake zake!
"Sikiliza cwty heart najua umejisikia vibaya mama kama ningekua sikupendi nisingekua nawe hapa saivi"
"Mke wangu yuko nyumbani akijua akijua niko kazini ila kutokana na penzi langu kwako niko nawe hapa saivi ebu tuliza presha mpenzi uku akiwa anampapasa kumtuliza presha mara gafla
* * * Hance ebu shukuru basi tule!
"Mama jamani siushukuru wewe ndie umeandaa! Ebu acha utani shukuru!
"Asante bwana yesu kwa riziki uliyotupatia ukambariki kila mmoja atakayeshiriki hata yule aliye andaa pia ukampatie baraka na nguvu"
"Nina itakasa kwa damu ya Yesu ikawe nguvu na afya milini mwetu Ameen!!
"Tukaanza kula uku Mama akiwa anamtazama Aurelia siakaanza utani wake!
"Natamani iwe familia mmoja katika familia yangu!
"Mama unamaana gani kusema ivyo!
"Natamani Aurelia aje kua mkwe wangu siitapendeza iwe kwa Moses au Hance"
"Ha ha ha ha ha itapendeza mama ila ni mipango ya Mungu hiyo uwezi jua kama Mungu akipanga akuna awezaye kupinga"
"Aurelia nae akawa amtia faraja mama kwa njia ya mafumbo!
"Nikajikuta nacheka kimoyomoyo uku najisemea angejua uyu ndie mkwe wake "
Basi wakati tunakula nikajikuta namchokoza Aurelia kwa kumkanyaga kanyaga miguu"
"Tukiwa tumekaa mezani Aurelia na mama wakiwa wamekaa upande wao uku mimi na Mose tumekaa wetu tukiwa tuna tazamana"
Taratibu tena nikaanza kumgusagusa Aurelia uku nikimtekenya tekenya na vidole"
"Akanitazama uku akinitaka niache hako kamchezo!Mimi ndio kwanza nikawa nimenogewa"
"Baada ya kuona tutagundulika akanifanyia makusudi akaikunja miguu weeh!
"Sangapi nisianze kumchezea Mama hadi nae akashtuka na kusema !* * * Mustapha akiwa anambembeleza mpenzi wake mara gafla mchupuo wake mwingine ukapiga simu"
"Nani uyo ni mke wako?
Hapana ni namba ngeni sijui ni nani?
"Pokea weka Loudspeaker ni sikie ni nani uyo!
"Hallow!
Niambie darling uko wapi nimekumic sana mpenzi na hamu nawe!
"Mustapha akiwa ameshikwa na kigugumizi na kushindwa kuji akiwa amebakia kusema uko wapi! Uko wapi?
"Yule mwanamke akamnyang"anya simu nakuanza kumporomoshea matusi mfululizo bila hata salamu"
"Wakiwa katika mparangano wa kunyang"anyana simu kati ya Mustapha na yule binti mara gafla ikadondoka wallet ya Mustapha kitandani yule mwanamke alipoiona akailalia pasipo Mustapha kujua na..........,...ITAENDELEAAAAAAAA
WEKA TANGAZO

0 maoni: