STORY: THE WORLD IZ NOT FAIR MTUNZI: CHICOLOVE JR NAMBA: 0658,0765, 270133 SEHEMU: 5

WEKA TANGAZO Hey mbona unamwangalia sana uyo dada
"Je mnafahamiana? Nikajikuta nimeshtuka hadi yule binti nae akabaki akiniangalia machoni nakuzidi mfanya boyfriend wake azidi kuchanganyikiwa!
"Hakika mtakua mnafahamiana Aurelia do you know dic boy?
"Aurelia akabaki anamshangaa uku akisema ngoja tumsaidie kwanza mambo mengine yatafuata!
"Fuck! Fuck am ask you who iz he?
"Junior calm down watz wrong with you?
"Are you cheat me? Who iz he ?
"Aurelia akawa anamtazama tu uku uso wake ukiwa umejaa hasira pasipo kumjibu chochote!
"Junior akaendelea kufoka kwa hasira uku akitoa matusi akapanda kwenye gari na kuondoka!
"Akaniacha pale na Aurelia akiwa ananisaidia akaniweka pembezoni mwabarabara na kuniambia!
"Hance naomba nipe dakika tano nichukue vocha hapo mbele nakuja sasa ivi take care ok usijali achana na yule mpuudhi"

"Baada ya kuniacha pale nikaanza kulegea taratibu na njaa niliyokua nayo ikazidi kunipelekesha uku nikiwa najiuliza nini kitatokea kati ya Aurelia na Junior!

"Aurelia akarudi akiwa amebeba juice uku akiwa anaongea na simu kama vile anampa mtu habari za hatari!
"Hey Hance usijali dada yangu anakuja hapa sasa ivi kutuchukua tuende hospital naomba uvumilie tu!
"Moyo wangu ukaniuma gafla nakujikuta najutia ile kauli ya kuwachukia wasichana wote duniani ndani ya nafsi nikaomba kimoyomoyo Mungu anisamehe kwa kile nilichokitenda!
"Mawazo yakaenda mbali zaidi nikawa nimetulia tu kimya!
"Hey Hance unawaza nini usijali anakuja saivi tunaenda hospital!
"Taratibu Aurelia akawa amenishika bega uku akiwa anaongea sauti ya upole kwangu kama ananibembeleza!
"Akaanza kunyoosha nyoosha mkono wangu kuupa mazoezi nakunifanya nizidi kumtazama kwa hisia kali uku moyo wangu ukiwa umeshikwa na mshangao fulani ivi!
"Nikajikuta nami nimenyanyua mkono wangu nikamshika shavu na kumwambia!
"Je unafuraha? Uku nikiwa namtazama kwa makini sana macho yake!
"Ndio Hance kwanini umeniuliza swali hili?
"Uso wako unaonyesha umekosa furaha najua ni kwa sababu gani ila usiogope kila jambo linawezekana!
"Mmmmh!akashusha pumzi kisha akainama pasipo kujibu chochote!

Wakati akiwa ameinama pale gafla simu yake ikapigwa akainuka haraka na kuniambia Hance amka twende hospital!
"Dada njoo basi tumsaidie ameumia!
"Kwani tatizo ni nini?
"Nikiwa najifuta futa vumbi pasipo kumtaza dada yake Aurelia!
"Ile nimeinua tu macho tukakutana uso kwa uso kila mmoja akabaki anamshangaa mwenzake!
"Nikamgeukia Aurelia nakumuuliza uyu ni dada yako wa tumbo moja?
"Ndio Hance kuna tatizo gani kwani?
"Hapana uyu binti namfahamu!
"Umemfahamia wapi?

"Nikashindwa kujibu nakujikuta namtazama dada yake Aurelia machoni uku nikiwa.............ITAENDELEAAAA!!!
WEKA TANGAZO

0 maoni: