FURSA ZA NDOA NA UMRI WA WANAWAKE

0 maoni
Poleni Sana madada wa zama hizi wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea. Mliochezea fursa.
1. Ulivyokuwa una miaka18 mpaka 22 walikuja waposaji ukasema bado unasoma. Au Wazazi wako walikwambia huwezi kuolewa bado unasoma na hujapata msingi wa maisha. Ulisahau kama ambavyo walivyosahau kuwa maisha anapanga Allah na rizki haina mahusiano na elimu. Mkasahau kuwa unaweza ukaolewa na masomo yakaendelea.
Pole Sana Dada yetu.
2. Kweli ukaendelea na masomo lakini ulivyofika form four au six ulifeli mtihani. Au ulifaulu lakini sio kwa kiwango ambacho ulitarajia ukalazimika urudie mtihani au usomee kitu ambacho hukukitaka. Au ukafika chuo kabisa lakini ukafeli. Au ukafanikiwa kumaliza chuo. Kwakuwa ni binti unapendeza na ndoa ilikataliwa walikuja wachumba wasio rasmi (maboy friend). Na ulikuwakubalia maskini. Wakachill sana mkachat sana na mkatoka out. Kumbe walikuwa wanakupotezea muda tu.
Poleni Sana Dada zetu.
3. Ukafika chuo kikuu ukaanzisha mahusiano na kijana mkawa na ndoto za ndoa. Na wakaja watu wengine kuposa. Ukajibu una mtu wako. Tena kwa mbwembwe ukasema una mpenda sana (mahaba niue). Ukabaki kila siku unabadilisha profile yako kutilia mkazo kuwa umezama kimahaba. Ukasahau kuwa uchumba ni mwanamume kuja nyumbani na akakubaliwa. Kumbe alikutamani tu moyoni ulikuwa haumo ndio maana hakuona haja ya kuleta posa.
Poleni Sana Dada zetu.
4. Uliwakatalia wengi wenye sifa nzuri za kukuoa kwasababu yake. Una maliza chuo ukiwa na miaka 27 au 28. Wale wote waliokuja kutaka kukuoa washaoa. Matokeo yake unapoteza imani na wanaume wote. Hali ya kuwa kosa ni lako.
Pole sana Dada yetu.
5. Walikuja wenye kukuposa ukasema hawana hadhi kama yako. Unataka msomi mwenzio. Au awe na mali. Ukasahau kuwa mwanaume mwenye mafanikio huwa nyuma yake kuna mwanamke makini sana. Na hukutaka umakini huo ukitaka uzikute tu hizo mali.
Pole Sana Dada yetu.
6. Upo kazini mwaka wa tatu hajaja mchumba. Una miaka 30. Wote Wanaokuja wanataka wakate matamanio yao ya kimwili tu. Na ukikumbuka ulitoa mimba kadhaa wakati unasoma kwa kuwa hukutaka mimba hiyo. Itakuharibia malengo yako ya kielemu.
Pole sana Dada yetu.
7. Walikuja watu wakitaka kukuoa ndoa ya uke wenza ukasema hutaki kusikia upuuzi huo. Ni bora usiolewe lakini kuolewa mitala ni nuksi Kwako. Unataka mume wa peke yako. Kuolewa Mitala ni mambo ya kizamani ukasahau kuwa hata bibi yako mzaa babu yako alikuwa ni mke wa nne kama si watano wa babu yako.
Jambo ambalo ulishindwa kulifahamu Dada yetu, ni kuwa huu ulimwengu waoaji ni wachache sana. Wengi ni mafukara sana, wengi ni wazinzi sana sio waoaji, wako mashoga sio waoaji, Wapo walioathirika sio waoaji, Wapo ambao ni wagonjwa wasio weza kuhimimili ndoa………….. Na waolewaji mko wengi Sana.
Maskini Dada yetu ulishindwa kufahamu kuwa ulimwengu wa Leo Waume ni kushare kama sio kwa njia ya Halali basi itakuwa kwa njia ya haramu.
Pole sana Dada yetu.
8. Sasa Leo umri umeenda huna kazi hata pesa ya kununua mahitaji ya kike huna. Wachumba uliokuwa unawaona wa nini Leo unajiuliza utawapata vipi. Masomo Umemaliza kazi hakuna. Ndoa za wake wengi ulizozikataa Leo unazitamani lakini hakuna hata anaekuuliza hali.
Umeamua ujiachie mitandaoni labda kutapatikana mchumba. Kila ajae anataka akuchezee tu.
Au kazi unayo nzuri lakini hakuna mume wa ndoto zako wote wajao wanaitaka mali yako tu. Sasa unaamua ujitafutie mtoto wa Zinaa kwa hoja kuwa una mali zako. Maskini Dada pole sana. Maamuzi ya mtu yalipoteza muelekeo wa maisha yako.
Umebaki umejiinamia hujui Unafanyaje pole sana Dada yetu. Ulisahau kuwa ujana ni maji ya moto. Lakini ujana wa mwanamke ni maji ya moto yaliyomo kwenye chumba cha barafu. Au mlisahau usichana ni biashara ya nyanya.
Wale wote ambao uliona washamba kwa kukubali ndoa mapema wamo ndani ya Ndoa zao. Wanaitwa mama mwenye watoto wanaofahamika baba zao. Maisha yanawaendea. Na wako vizuri tu kimaisha.
Pole sana dada yetu

NAMNA YA KUMTAMBUA MWANAMKE MPUMBAVU NA MWANAMKE MWEREVU

0 maoni
MWANAMKE MPUMBAVU
1.Anamkomoa mumewe
2.Analala mapema kabla ya mumewe
3.Anachelewa kuamka kabla ya mumewe
4.Mbishi, anahic kuonewa mda wote
5.Anadhani kumnyima mumewe unyumba ni
kumkomoa
6.Mmekaa sebuleni anahadithia tu
Mafanikio ya familia za wa2
Wakati ye ndo kigezo cha kero.
7.Hataki kuzungumzia mshara wake
8.We unajenga family ye anajenga
Kwao
9.Mkikaa 2 anaanza umbea kuponda
Ndugu na majirani
10.Haridhiki (mwanaume unatoa jasho
ila ye anakudiscourage wakati
Ye akishuka kwenye kochi anakaa
Kwenye jamvi na baadaye anelekea
saloon kupiga umbea kuhusu mama
joyce kafumaniwa gesti.
11.Nyumbani housegirl hapumziki.
12.Anajali ajira yake hataki
kufuatiliwa mambo yake.
13..Anakera sana, cwezi kuacha kazi
yangu hata km anaumwa, kajikata
kucha halafu anadai apelekwe Agha
Khan au India.
NOTE: akikutana na mwanaume
kichwa ngumu anamrudisha kwao
ameshazalishwa watoto 3, anaenda
kwa mwingine anaongezewa watoto
2, anazinguliwa anapigwa toto lingine
mmoja mtaani, unakuta kazaa na kila
familia mtaani baadaye anaishi ghetto
au kwao.
MWANAMKE MWEREVU.
1.Unaamka yeye kashaamka na
kusema "baby amka maji ya kuoga
yapo bafuni" (mwanamke adimu sana)
2.Unajiandaa kwenda kazini khaa, nguo
zishapigwa pasi (jamani hiyo kazi
kafanya saa ngapi? unajikuta unaenda
kazini upo kwny daladala kimoyo
moyo unamwambia "I love u honey"
3.Unarudi jioni unakuta anakuvua
soksi acha 2 hujui hata anazifua saa
ngapi maana huwa hujui anazifua saa
ngapi?
4.Umejipumzisha kwny kochi au kitandani mara
kakukalia
Mgongoni anakufanyia masej
Mgongoni, khaa alijuaje unataka
Ufanyiwe masej? Unaishia kusema
Thanks baby.
5.Kila anachotaka kufanya
kujiendeleza anakuambia na unaweza
kumpa mtaji mana ni mkweli (ni
baraka kwny familia)
6.Anapenda ndugu zako (cyo mama
mkwe akija anasimamisha pua juu
km kitimoto)
7.Anakupa moyo kwny wakati
mgumu, mf: umefukuzwa kazi
anakushauri (baby hayo ni maisha
tu, ucjal utafanikiwa km vp 2cmamie ule mradi
wangu mpk
uajiriwe) khaa jamani yupo km huyu
fb? Upareni? Uchagani? Usukumani je?
8.Ukirudi nyumbani unakuta
anamfundisha mtoto wako maadili ya
kimungu (wow heri 2zae 2 wa pili)
9.Anakufariji…Baby usiogope ni
mapito ya dunia, jikaze mume
wangu, nipo upande wako), heheeee
hata ukinuna unabembelezwa.
10.Mwenye kushukuru na
suprises, hawezi kukusahau, (baby hii
zawadi kwa ajili yako,umenisaidia sana
mume wangu, u change my
life, "baby leo birthday yako, khaa
unaona keki mezani"),kuna mke km
huyo?
11.Ana uhakika mimba yako ("baby
nina suprise, kumbe mwezi uliopita
ulinipa toto, nina mimba yako (cyo ooh
khaaa 2mefanya mapenzi juzi 2
umenipa dragon mwingine)
NB. Mwanamke km huyu ni
blessing, kila jioni unaona toto zako
zimekaa kwenye kochi yaani vitoto
vizuri miguu mifupi hata vikikaa
kwenye kochi miguu hazifiki kwny
sakafu vinaangalia cartoons.
Hehehe ni mtazamo tu…

Jinsi ya kumfanya mwanamke afurahi na akupende kwa kumfanyia mambo anayoyataka

0 maoni
Kuna mambo ya msingi ambayo mwanamke anahitaji kutoka kwa mwanamme ili kufurahi na kutulia katika mahusiano japokuwa sio rahisi kukwambia mojakwa moja.

Mambo hayo ni kama ifuatavyo;

Kupewa nafasi na kipaumbele.

Wanawake wanapenda kuwa namba moja au kupendwa kuliko yeyote. Kumpenda mwanamke haikuishii kwenye kumpata na kumliki, kisha kujisahau kwa kisingizio kuwa umemuoa au umemvisha pete ya uchumba, ni zaidi ya hapo. Wanawake wanapenda watangulizwe katika mapenzi na kusiwepo na mwingine wa kuchukua nafasi yao katika mazungumzo na mapenzi kwa ujumla na katika maisha yao.

Kuheshimiwa

Wanawake wanapenda kueshimiwa kwa maneno na matendo. Wanawake hawapendi kuitwa majina mabaya kwa mfano mjinga, Malaya au kulinganishwa na wanawake wenzao wabaya. Wanawake hawapendi kukosewa heshima hasa mbele za watu, hata kama ni kwa mambo madogo madogo.

Kuridhishwa Kwenye tendo la ndoa

Mwanamke anapenda aridhishwe Kwenye tendo la ndoa. Hata kama utakuwa na kiwango kikubwa cha mapenzi juu ya mpenzi wako kwa kiwango gani, ukiwa dhaifu katika tendo la ndoa utayumbisha penzi lako. Utundu na ufundi unahitajika ili kumkata kiu mpenzi wako. Mwanamme anatakiwa kuhakikisha kuwa anamtosheleza mpenzi wake katika tendo hilo.

Nafasi ya kuongea na kujieleza

Wanawake wanapenda wapewe nafasi ya kuongea na kujieleza vile watakavyo. Mpe uhuru mpenzi wako kuzungumza na kumsikiliza bila kumkatiza kwa ukali pale anapoongea sana. Kwa kawaida wanawake wanatajwa kuzungumza maneno 25,000 kwa siku, wakati wanaume wakibaki na kiwango cha maneno 5,000 kwa siku, wanawake hupenda zaidi kujieleza walivyo mbele ya wengine. Kwa hiyo wakizuiwa wasiongee hujiona kama wanakosa nafasi muhimu ya kueleza mawazo yao.

Kusaidiwa katika shida na matatizo yao

Wanawake wengi hutegemea kuwa wanapokuwa na wapenzi watasaidiwa katika matatizo ya kimaisha na migogoro ya kimawazo. Kwa mfano ushauri juu ya maisha yao, kulindwa na hatari za kimaisha, kusaidiwa katika shida na kuongozwa pale wanapohisi kushindwa kufanya jambo. Kama mwanaume hatamfanyia mpenzi wake hili atakuwa amekosa sifa za kuteka penzi la mwanamke.

Kubembelezwa

Wanawake hupenda kubembelezwa hasa pale wanapokuwa na huzuni. Wanawake wengi hupenda kuelimishwa zaidi kuliko kufokewa. Wanawake hawapendi kukaripiwa, mara nyingi hupenda kuungwa mkono wanapokuwa na misuguano na wengine. Ili mwanaume amteke kimapenzi mwanamke lazima awe nyuma yake hata kama atakuwa na kosa.

MADHARA SABA KWA WANAUME WAOPENDA KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE

0 maoni
Kama nilivyoelezea kwenye mada za wiki kadhaa zilizopita, mchezo huu unatumika sana katika mapenzi ya sasa, watoto wa mjini wana usemi wao kwa kitu kilichovuma kuwa ‘ndiyo habari ya mjini’.

Mchezo huu umekuwa ukipendwa sana na wanaume wengi ambao wengi wao huwa hawatumii kinga na kusababisha wengi kupata magonjwa ya zinaa pamoja na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Lakini mchezo wa kuruka ukuta umekuwa na madhara makubwa sana kwa wanaume wanaoufanya kwa muda mrefu.

Tulipoangalia upande wa wanawake, tuliona sehemu kubwa ya wanaopenda mchezo huu ni wanaume ambao wengine wamebatizwa majina ya ‘basha’, wakimaanisha mwanaume mpenda kuruka ukuta bila kuangalia ni wa mwanaume mwenzake au wa mwanamke.


Kwa vile nia ya kona hii ni kuelimisha madhara ya mtu kupenda kuruka
ukuta ili aache mara moja, tunaendelea kutoa elimu ya bure ili mtu yakimkuta ajue yamempata kwa kiburi chake na kwa kupenda starehe ya kipuuzi.

Madhara anayoyapata mwanaume anayependa mchezo huo ni kama ifuatavyo:

Kwanza: Husababisha kusinyaa au kuweka makovu kwenye njia ya haja ndogo.

Pili: Njia ya haja ndogo kuziba kiasi au kuziba kabisa.

Tatu: Kupata saratani (kansa) ya tezi za figo (prostate gland).

Nne: Kupata magonjwa sugu ya uti wa mgongo.

Tano: Kuharisha.

Sita: Maambukizi ya VVU ambapo mwisho wake ni Upungufu wa Kinga Mwilini (Ukimwi).

Saba: Baadaye mhusika kupata msongo wa mawazo au sonona kwa kujutia tendo hilo.

Nina imani ndugu yangu umeona madhara mabaya sana ya tabia hiyo mbaya. Inawezekana umezoea mchezo huo wa kuwaingilia wenzako na kuona raha lakini tumeona madhara yake, ambayo kwa hakika kama wewe ni mmoja wao, unatakiwa kuacha mara moja kwa vile mwisho wake ni majuto na mateso.

Jiepushe kuiga mambo bila kujua faida na hasara zake pia usimtie mwenzako majaribuni kwa kumlazimisha kuingia kwenye mchezo huo. Wanawake wengi wamekuwa wakilazimishwa na wanaume kuingiliwa kinyume na maumbile kwa kuwatishia kuwaacha kama watakataa.
Swali linakuja, kipi bora, kuharibiwa au kuachana?
Kumbuka baada ya kuharibikiwa, thamani yako hushuka na sifa yako ikiwafikia waharibifu wa watu, basi unageuzwa jamvi la mtaa na hatimaye unakufa kwa msongo wa mawazo au mateso ya ugonjwa utakaupata baada ya kukubali kuingiliwa kinyume na maumbile.

Unaweza kushangaa baada ya kuelezea madhara yanayowapata wanaume nimehamia kwa wanawake. Ukweli mchezo huu umewaathiri sana wanawake ambao wengi wanaujutia.

Unajua Wanaume wanapenda kuoa Wanawake wa aina gani?

0 maoni
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku.
Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. 
Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. 
Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

 
MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. 
Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha  siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.
Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
 
Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya  maisha ya  ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia  ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.
 
WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini  wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa  anatabia mbaya.
Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya  wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume  ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.
 
WENYE UCHU NA MAENDELEO
 
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini. 
Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.
 
WASIOPENDA MAKUU
 
Kuna  wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"
  
Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama  ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho  nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

 
Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa  kuwaoa.  Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa  tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi  ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema. 
Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.
 
WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.
Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
 
Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
 
Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.
Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
 Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam.

 Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

Jifunze kumsifu Mpenzi wako akupe mazuri zaidi

0 maoni

YAPO mengi mazuri ambayo huenda mpenzi wako aliwahi kukufanyia, je uliwahi kumshukuru kwa kukufanya ufarijike? Naamini Mungu amekujaalia kuwa na mpenzi mzuri, mwenye kila sifa ambayo ulitamani awe nayo, je ulishawahi kumsifia hata kwa kumwambia ni mzuri?
Huenda ulishawahi kufanya hivyo lakini kwa taarifa yako wapo ambao wanahisi kufanya hivyo eti ni ulimbukeni. Ulimbukeni? Kumsifia mpenzi wako  unaona ni ulimbukeni wakati wataalam wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa, wanawake ni watu wanaopenda kusifiwa sana hata kwa madogo wanayoyafanya?
Unaona hatari gani kumsifia mpenzi wako kuwa ni mzuri? Unadhani unatumia nguvu gani kumsifia mpenzi wako kutokana na mahaba mazito anayokupata?
Kwa taarifa yako unaweza kuona ni kitu kidogo sana  lakini madhara yake kwenye penzi ni makubwa.
Kumsifia mpenzi wako kwa yale anayokufanyia kuna faida nyingi sana lakini kwa leo nitagusia chache. Kwanza kunaongeza mapenzi. Mume/mke anaposifiwa kuwa anajua mapenzi hata kama si kwa kiwango kikubwa, anafarijika sana.
Unapomwambia mpenzi wako: ‘Dear nashukuru kwa mapenzi uliyonipa jana, umenipa furaha ya ajabu ambayo siamini kama kuna mtu mwingine wa kunipa, nakupenda sana’.
Maneno kama haya hutumii nguvu wala muda mwingi kuyafikisha kwa mpenzi wako lakini uzito wake ni mkubwa. Kwanza anajihisi aliyekamilika kwa kufikia hatua ya kufanya mambo yakamridhisha mpenzi wake na kwa mazingira hayo anaamini huwezi kumsaliti. Hisia hizo zitamfanya azidi kukupenda.
Hilo ni kwa wote yaani kwa mwanaume na mwanamke. Lakini pia unapomsifia mpenzi wako kwa yale anayokufanyia, unamfanya aongeze kasi ya kukufanyia ili nawe uzidi kumpenda.
Kwa mfano, unapokutana na mpenzi wako kisha ukamwambia ‘umependeza kweli mpenzi wangu, nazidi kukupenda kwa unavyovaa’.
Mtu anayeambiwa maneno haya atajitahidi sana siku zote aonekane nadhifu na wa kuvutia kwa mpenzi wake akijua kwamba, akivaa ilimradi kuvaa, hatamfurahisha mpenzi wake. Kwa maana hiyo kumsifia mpenzi wako kunamfanya azidi kuwa bora.
Lakini kusifia kusiwe kwa kinafiki. Usimsifie mpenzi wako eti ili kumfanya ajione bora kumbe katika uhalisia siyo hivyo.
Tusifiane pale inapobidi huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo tutapata faida. Tusiwe na tabia ya kuchukulia poa kila tunachofanyiwa na wapenzi wetu.
Kama kakuridhisha kimapenzi, msifie kwamba yeye ni muhimu kwako kwa kuwa amekupa ulichotarajia. Amekupikia chakula kizuri, msifie kuwa yeye ni mpishi mzuri. Hiyo italinogesha penzi na utashangaa kila siku inayokwenda kwa Mungu penzi lenu linachanua.
Lakini mbali na hayo, unatakiwa kuridhika kwa kile unachokipata kutoka kwa huyo mpenzi wako ulinaye kwa sasa. Najua kwenye uhusiano wengi tumetoka mbali. Wapo waliowahi kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja huko nyuma na kila mmoja alikuwa na kiwango chake cha kukuridhisha.
Inawezekana kuna ambaye unamkumbuka kwa mapenzi mazito aliyokuwa anakupa zaidi ya huyo uliyenaye. Hiyo ni historia, imepita! Kama huyo uliyenaye si mtaalam sana wa kukufikisha pale unapopata, ridhika na hicho kidogo unachokipata endapo atakuwa anaonesha kukupenda kwa dhati.
Mpe moyo, msifiesifie kidogo kwa hiyo furaha kiduchu anayokupa huku ukiamini kuwa, atabadilika kadiri siku zinavyokwenda.
Kumbuka cha msingi katika maisha yetu ni kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli na si kumpata anayeweza kukuridhisha katika mambo kadha wa kadha.

Wanaume mnajua hili: Mfanyie mwanamke akuzidishie raha

0 maoni
 MAMBO vipi ndugu zangu? Ni furaha yangu kwa mara nyingine tena kukutana nanyi wapendwa wasomaji wa safu yetu hii. Tumshukuru Muumba wetu kwa kutujaalia uhai na afya njema, lakini zaidi ya hapo tumshukuru pia kwa kutuumbia kitu mapenzi au siyo jamani?
Siku zote hatutaacha kuzungumza juu ya mapenzi kwani ni ukweli usiopingika kwamba mapenzi ndiyo maisha yetu.
Tunafanya kazi usiku na mchana, tunahangaika huku na huko, lakini mwisho wa siku tunafikiria jinsi gani tutapata kuboresha na kufurahia maisha na wapenzi wetu.
Tunafikiria pia ni jinsi gani tunaweza tukapata utulivu na amani katika maisha ya kimapenzi na wapenzi wetu, waume zetu au wake zetu katika siku zote za maisha yetu.
Ndugu zangu, Mungu ametuwekea mapenzi ili tupate raha na amani katika maisha yetu.
Kwa maana hiyo, wale wanaoyachezea na kuyavuruga mapenzi kwa makusudi kwa kuumiza hisia za wenzao kisha kuwasababishia vilio si watu wa kupendeza mbele ya macho ya wale wanaojua hasa nini maana ya mapenzi.
Wanawake ni watu wa kuheshimika na kupewa furaha wanayohitaji. Unapompata mwanamke anayekupenda na kukuheshimu, huna sababu ya kumfanya ajute kuwa na wewe.
MPENDE NA MTHAMINI!
Yawapasa wanaume mfahamu kuwa, wanawake ni zawadi kwenu, pumziko na tulizo la mioyo yenu. Wanawake ndiyo raha na amani kubwa ya maisha yenu.
Kosa kubwa mnalofanya wanaume ni kuutumia vibaya mfumo dume hasa katika suala nyeti kama mapenzi.  Mapenzi si ubabe, mapenzi ni upole na ukarimu.
 Pamoja na kwamba mmebarikiwa kwa kupewa nafasi ya kuwa kichwa katika nyumba lakini linapokuja suala la kurekebisha tofauti zinazojitokeza katika uhusiano wenu, si vyema kutumia njia za kibabe.
Niwaambie kitu, wanawake ni wa hisia zaidi na waliobarikiwa kuwa na upendo wa hali ya juu na ndiyo maana wakapewa dhamana ya kubeba mtoto tumboni kwa miezi tisa na pia kumnyonyesha na kumlea kwa miaka kadhaa, wewe mwanaume ungeweza?
Nasema ni watu wa hisia kwa sababu, hivi uliwahi kufikiri ni kwa nini wanawake huridhika na kujisikia poa kweli wanapopewa zawadi kama ya maua na kadi zenye ujumbe wa mapenzi ukilinganisha na wanaume?
Unafikiri ni kwa nini wana machozi ya haraka wanapotendwa? Au unafikiri ni kwa nini wanapenda kutumiwa ‘love sms’ zaidi kuliko kupigiwa simu? Jiulize.
Mimi nawaona wanawake kama watu wa kuheshimiwa na kupendwa kwa dhati.  Mkumbuke wanawake ndiyo mama zetu, walezi wetu na ndiyo nyumba zetu. Jaribuni pia kujicontroo na huo mnaouita ukijogoo kwamba eti ninyi ni watu msioridhika na mpenzi mmoja.
Jaribuni kufanya kila mnaloweza kuifuta ile dhana ya kwamba wanaume hawaaminiki hata kidogo. Ridhika na mpenzi uliyenaye, heshimu hisia zake na thamini mapenzi yake kwako na mpe ile kitu roho inapenda!
Ni hayo tu kwa leo.